9 wakamatwa kwa ulaghai wa shilingi bilioni 1.5

Washukiwa ambao ni maafisa katika Wizara ya Fedha wanazuiliwa katika makao makuu ya EACC jijini Nairobi wakisubiri kufikishwa mahakamani kesho Jumatano.

Martin Mwanje
0 Min Read

Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi, EACC imewakamata washukiwa 9 kutoka Wizara ya Fedha kama sehemu ya uchunguzi wa madai ya ulaghai wa shilingi bilioni 1.57. 

Washukiwa hao waliokamatwa  kuhusiana wanazuiliwa katika makao makuu ya tume hiyo jijini Nairobi.

EACC inapanga kuwafikisha mahakamani kesho Jumatano, Agosti 19.

 

Share This Article