Rais wa Senegal amfuta kazi Waziri Mkuu Sonko

KBC Digital News
2 Min Read

Rais wa Senegal Bassirou Diomaye Faye amemfuta kazi Waziri Mkuu Ousmane Sonko, kwa kutumia amri ya rais siku ya Ijumaa.

Uamuzi huo uliotangazwa kwenye runinga ya serikali unamaliza miezi kadhaa ya kile kinachoonekana kuwa mzozo wa madaraka na mvutano kati ya Rais Faye na Waziri Mkuu Sonko.

Waziri Mkuu Sonko, ambaye ni maarufu miongoni mwa vijana alimchagua Faye kama mbadala wake kwa uchaguzi wa urais wa 2024 baada ya kuzuiwa kugombea.

Kufutwa kazi huku kunafuatia msururu wa maswali na majibu katika Bunge la Kitaifa ambapo alimkosoa waziwazi Rais Faye.

Mamia ya wanafunzi kutoka UCAD (Chuo Kikuu cha Cheikh Anta Diop) waliingia kwenye mitaa ya Dakar kuonyesha kumuunga mkono Ousmane Sonko.

Sonko alitangaza kwenye mtandao wa X kwamba anaweza kulala kwa amani usiku wa jana.

“Alhamdulillah. Usiku wa leo nitalala nikiwa na amani katika mtaa wa Keur Gorgui.”

Hivi majuzi, Ousmane Sonko mwenyewe alikuwa amedokeza uwezekano wa kurejea kwa upinzani.

Ousmane Sonko na chama chake walishinda viti 130 kati ya 165 katika Bunge la Kitaifa.

Mnamo Jumanne, Aprili 28, Wabunge wa Senegal walipitisha marekebisho ya vifungu viwili vya kanuni za uchaguzi, kuruhusu watu waliopatikana na hatia ya makosa madogo kushiriki katika chaguzi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Ousmane Sonko, kwa uchaguzi ujao wa urais mwaka wa 2029.

Taarifa ya BBC.

Share This Article