Wafanyakazi wa OLA Energy kutimuliwa kutokana na makali ya uchumi

Dismas Otuke
1 Min Read

Kampuni ya mafuta ya OLA Energy, inatarajiwa kutimua idadi ya wafanyakazi isiyojulikana katika mikakati ya kukabiliana na hali ngumu ya  kiuchumi.

Taarifa ya kampuni hiyo imesema hali ngumu ya kiuchumi imeongeza  gharama ya biashara na hawana budi  kuratibu upya biashara zao kote nchini, na hali hiyo itasababisha kusimamishwa kazi kwa baadhi ya wafanyakazi wake.

Kampuni hiyo pia imedokeza kuuza baadhi ya vituo vyake vya mafuta viungani mwa  jiji la Nairobi.

Itakuwa mara ya pili kwa OLA Energy kuwafurusha wafanyakazi wake baada ya kuwalazimu maafisa wake 189 kustaafu mwaka 2019.

OLA Energy ina  wafanyakazi zaidi ya 1,500 katika kaunti 17  nchini.

 

Share This Article
Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *