Waakilishi wanne wa Afrika watashuka uwanjani kuanzia usiku wa manane Jumatatu, kwa mechi za ufunguzi za Kombe la Dunia linaloendelea.
Tembo wa Ivory Coast wanaorejea kwenye kipute hicho baada ya miaka 12 ,wataanza harakati zao kundi E, dhidi ya Ecuador ya Amerika Kusini.
Mechi hiyo itachezwa katika uwanja wa Philadelphia.
Ivory Coast watalenga kuondoa nuksi ya kupoteza kila mechi ya Kombe la Dunia wanapocheza na wapinzani wa kutokea Marekani Kusini.
Baadaye saa kumi na moja Alfajiri itakuwa zamu ya The Carthage Eagles ya Tunisia, kukabiliana na Uswidi, uwanjani Monterrey,nchini Mexico.
Tunisia wanashiriki Kombe la Dunia kwa mara ya tatu mtawalia.
Uhispania ambayo inaorodhoshwa ya pili bora duniani itamenyana na waakilishi wa Afrika Cape Verde, wanaoshiriki kwa mara ya kwanza katika kundi H.
Mchuano huo utachezwa katika uwanja wa Mercede Benz kuanzia saa moja usiku.
Hatimaye saa nne usiku ,Ubelgiji na Misri watakutana kwa mara ya kwanza katika historia katika mechi ya kundi G nchini Marekani.