Kenya Pipeline wajaa nusu fainali, Prisons, KCB wajikwaa

Pipeline watashuka kucheza nusu fainali leo jioni dhidi ya Zamalek walioIbandua KCB seti 3-1 katika robo fainali jana.

Dismas Otuke
1 Min Read

Kenya Pipeline ndio timu pekee ya humu nchini iliyofuzu kwa nusu fainali ya Kombe la Afrika kwa wanawake, mashindano yanayoendelea mjini Abuja, Nigeria.

Pipeline waliicharaza APR ya Rwanda seti 3-0 za 25-21, 25-17, na 25-14 katika kwota fainali ya jana na kulipiza kisasi cha kulemewa na APR katika mechi ya makundi.

Pipeline watashuka kucheza nusu fainali kesho jioni dhidi ya Zamalek walioibandua KCB seti 3-1, katika robo fainali jana Jumatano.

Nusu fainali ya pili itakuwa baina ya Carthage ya Tunisia dhidi ya Al Ahly ya Misri, baada ya Ahly kuwabandua Kenya Prisons seti 3-1 kwenye robo fainali ya jana.

KCB watamenyana na APR kuwania nafasi za 5 hadi 8  pia kesho o huku LTV ya Cameroon, wakimaliza udhia na Prisons ya Kenya.

Website |  + posts
Share This Article