Spika Wetang’ula atetea sheria za kudhibiti matumizi ya mitandao

Dismas Otuke
1 Min Read

Spika wa Bunge la kitaifa Moses Wetang’ula ametetea sheria mpya zilizopitishwa na Wabunge na kuidhinishwa na Rais William Ruto, akisema zinalenga kuleta ustaarabu mitandaoni , kuzuia itakadi kali  na  uchochezi mitandaoni.

Wetang’ula amesema haya siku ya Jumapili alipohudhuria ibada katika kanisa la Katoliki la St. Teresa’s Isanjiro mjini  Malava kaunti ya Kakamega .

Akikariri manufaa  makubwa yaliyoletwa na utandawazi wa mitandao kama vile biashara,mawasiliano na elimu serikali inalenga kuzuia matumizi mabovu kama vile sinema za ngono kwa watoto na uhalifu wa mitandaoni .

Wetang’ula aliandamana na kiongozi wa wengi Bungeni Kimani Ichung’wah, aliyekanusha madai kuwa serikali inalenga kubana uhuru wa kujieleza nchini.

Website |  + posts
Share This Article