Rais William Ruto amekutana na viongozi wa mashinani kutoka kaunti za Kisumu, Siaya, Homa Bay na Migori, huku akianza rasmi ziara ya siku nne katika eneo hilo la Nyanza.
Kwenye mkutano huo ulioandaliwa katika eneo la kutua kwa meli katika kaunti ya Kisumu ,Rais Ruto alizungumzia agenda za maendeleo ya eneo hilo na jinsi ya kuliinua kiamendeleo.
Kama njia ya kumuenzi kiongozi wa chama cha ODM hayati marehemu Raila Odinga, kwa kuimarisha ushirikiano baina ya chama hicho na UDA kupitia kwa serikali jumuishi.
Rais alitaja ufanisi wa serikali yake katika kipindi cha miaka minne iliyopita ikiwemo kukwamua miradi ya maendeleo,na kutimiza nyingi ya ahadi zake za kabla ya uchaguzi mkuu uliopita.
Awali Rais alihudhuria ibada katika kanisa la Voice Of Salvation And Healing kaunti ya Kisumu.