Rais  Ruto asaini kuwa sheria muswada wa Fedha wa mwaka 2025

Wasindikaji na wakulima wanatarajiwa kunufaika  kutoka na kuondolewa kwa ushuru wa bidhaa ghafi,na vifaa vya kupakia chai na kahawa.

Dismas Otuke
1 Min Read
Rais William Ruto, amesaini kuwa sheria muswada wa fedha wa mwaka 2025,kwenye hafla iliyoandaliwa mapema leo katika Ikulu ya Nairobi.
Sheria hiyo italeta mabadiliko kadhaa mapya  ingawa hakuna ushuru mpya ulioongezwa kwa bidhaa za kawaida za matumizi.
Wasindikaji na wakulima wanatarajiwa kunufaika  kutoka na kuondolewa kwa ushuru wa bidhaa ghafi,na vifaa vya kupakia chai na kahawa.

Aidha,sheria hiyo pia itashuhudia kujumuishwa kwa ushuru mpya kwa kamari na huduma za kidijitali.

Website |  + posts
Share This Article