Kaunti za Uasin Gishu,Nandi na Elgeyo Marakwet kwa pamoja zimezindua mashindano ya michezo ya kuadhimisha siku kuu ya Mashujaa tarehe 20 mwezi ujao.
Mashindano hayo yatafikia kilele Oktoba 20 punde baada ya sherehe za mwaka huu za Mashujaa zilizoratibiwa kuandaliwa na kaunti hizo kwa pamoja.
Waziri wa sualama wa kitaifa Kipchumba Murkomen ameongoza uzinduzi wa mashindano hayo yatakayowaleta pamoja viajana watakaoshindana katika fani ya Voliboli,soka,Riadha,Mpira wa Kikapu.
Murkomen amesema lengo la mashindano hayo ni kuleta pamoja vijana wa kaunti hizo na kuhimiza amani na kupeleka sherehe za Mashujaa karibu na wananchi walio mashinani.
Mashindnao hayo yataanzia ngazi ya Wadi tarehe 26 mwezi huu kabla ya kuelekea kwa yale baina ya kaunti Oktoba 19, kwa fainali ya Voliboli nayo fainali ya soka ipigwe Oktoba 2o.

Mbio za Iten Marathon zitafanyika tarehe 18 mwezi ujao huku kitita cha shilingi milioni 63 zikishindaniwa .
Hafla ilihudhuriwa na Magava wa kaunti hizo tatu wakiwa;Jonathan Bii wa Uasin Gishu, Wisley Rotich wa Elgeyo Marakwet na Stephen Sang wa Nandi pamoja na Wabunge Gladys Boss Sholei, Julius Melly, Joses Lelmengit, Paul Biego, Timothy Kipchumba, Phyllis Bartoo, Maryanne Kitany, Adams Kipsanai, Julius Rutto, Janet Sitienei na Gideon Kimaiyo.