Blinken akutana na emir wa Qatar kushinikiza upatanishi wa mzozo wa Gaza

Martin Mwanje
1 Min Read
US Secretary of State Antony Blinken meets with Qatar's Prime Minister and Foreign Affairs Minister Sheikh Mohammed bin Abdulrahman bin Jassim al-Thani in Doha on October 24, 2024. - Blinken arrived on October 24 to key Hamas mediator Qatar as he seeks momentum to end the Gaza war following Israel's killing of the group's leader. (Photo by Nathan Howard / POOL / AFP)

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken leo Alhamisi amefanya mazungumzo nchini Qatar, ambayo ni mpatanishi mkuu katika vita eneo la Gaza.

Blinken anatafuta kuzidisha kasi ya kusitishwa kwa vita hivyo baada ya Israel kumuua kiongozi wa kundi la Hamas.

Baada ya kukutana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu mjini Jerusalem, Blinken alielekea Saudi Arabia na kisha Qatar, ambako atatafuta kutathmini msimamo wa Hamas kuhusiana na makubaliano ya kusitisha vita.

Blinken “alijadili juhudi mpya za kuhakikisha kuachiliwa kwa mateka na kumaliza vita katika eneo la Gaza” na emir wa taifa hilo la Ghuba, Sheikh Tamim bin Hamad Al-Thani, ilisema Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.

Kisha baadaye alifanya mazungumzo na Waziri Mkuu Mohammed bin Abdulrahman bin Jassim Al-Thani, ambaye kwa pamoja watawahutubia wanahabari.

Hiyo ni ziara ya 11 ya Blinken katika eneo hilo tangu kundi a Hamas lililpofanya shambulizi nchini Israel Oktoba 7, 2023.

Hajaambulia chochote wakati wa ziara hizo.

Lakini chini ya wiki mbili kabla ya uchaguzi wa urais nchini Marekani, Rais Joe Biden amepata matumaini mapya baada ya Israel kumuua kiongozi wa Hamas Yahya Sinwar katika Ukanda wa Gaza.

 

Website |  + posts
Share This Article