Watu wanne wafariki katika shambulizi la Israel Beirut

Tom Mathinji and BBC
1 Min Read

Watu wanne akiwemo mtoto wameuawa katika shambulizi la anga la Israel karibu na hospitali kuu ya serikali kusini mwa Beirut, wizara ya afya ya Lebanon inasema.

Shambulizi hilo lilionekana kulenga maegesho ya magari ya Hospitali ya Chuo Kikuu cha Rafik Hariri, chanzo cha hospitali kililiambia shirika la habari la Reuters.

Wizara ya afya imesema watu 24 wamejeruhiwa.

Ilikuwa ni miongoni mwa mashambulizi 13 ya anga yaliyokumba Beirut kusini Jumatatu jioni.

Jeshi la Israel lilisema lilikuwa linashambulia vituo vinavyohusishwa na Hezbollah.

Msemaji wa Israel hapo awali alikuwa amewaonya watu kuhama kutoka maeneo kadhaa kusini mwa Beirut, hata hivyo hospitali ya Rafik Hariri haikuwa miongoni mwa maeneo yaliyotajwa.

Video kutoka kitongoji cha Dahiyeh kusini mwa Beirut, ambapo maeneo saba yatakayolengwa yalitangazwa mapema, zilionyesha wenyeji wakikimbia kwa magari na kwa miguu huku mashambulizi hayo yakianza.

Eneo moja lililotambuliwa kama shabaha ya jeshi la Israel lilikuwa takriban mita 400 kutoka uwanja wa ndege wa Beirut, ambao ndiyo pekee wa kimataifa unaohudumia Lebanon.

Vyombo vya habari vya ndani vilishirikisha picha za baadhi ya madirisha katika jengo la uwanja wa ndege ambayo yalilipuliwa katika mlipuko huo.

Israel haijatoa maoni yoyote tangu ilipotoa maonyo ya awali ya kuwahamisha.

TAGGED:
Share This Article