Vipusa wa Kenya kukabiliana na Nigeria,raundi ya 16 kombe la Afrika

Malkia Strikers ambao walishinda mechi zao mbili za kundi A watalenga ushindi ili kufuzu kwa robo fainali huku wakijizatiti kutetea ubingwa wao na kufuzu kwa mashindano ya Dunia mwaka ujao.

Dismas Otuke
1 Min Read

Timu ya taifa ya Kenya,Malkia Strikers itashuka uwanjani Kasarani Jumamosi jioni kwa mechi ya raundi ya 16   dhidi ya Nigeria katika mashindano ya kuwania Kombe la mataifa ya Afrika.

Malkia Strikers ambao walishinda mechi zao mbili za kundi A watalenga ushindi ili kufuzu kwa robo fainali huku wakijizatiti kutetea ubingwa wao na kufuzu kwa mashindano ya Dunia mwaka ujao.

Katika mechi nyingine za raundi ya 16   siku ya Jumamosi,Uganda watakabiliana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo  kuanzia saa saba ,kabla ya Algeria kumenyana na Senegal  saa kumi  kisha Kenya wafunge ratiba saa moja usiku.

Mechi zaidi zitachezwa Jumapili huku fainali yake ikipigwa  Septemba 5.

 

Share This Article