Takriban watu 144 wamekufa na 732 kujeruhiwa kufikia sasa nchini Myanmar, kufuatia tetemeko la ardhi lililopiga katikati mwa nchi hiyo.
Takwimu hizi zimetolewa na kiongozi wa kijeshi wa Myanmar Min Aung Hlaing, ambaye anasema takwimu hizo zinatarajiwa kuongezeka.
Akifafanua idadi hiyo mpya, kiongozi huyo wa kijeshi anasema watu 96 wamekufa huko Nai Pyi Taw, 18 huko Saigaing na 30 huko Mandalay.
Kuhusu waliojeruhiwa, 132 kati ya hawa wanatoka Nay Pyi Taw na 300 wanatoka Sagaing, na idadi bado inatathminiwa katika maeneo mengine – takwimu za kijeshi zinasema.
Tetemeko hilo ambalo pia lilikumba nchi ya Thailand, ilisababisha vifo vya watu watatu, kufuatia kuporomoka kwa jengo la ghorofa.