Wanariadha 35 wateuliwa kuiwakilisha Kenya Olimpiki

Dismas Otuke
2 Min Read

Chama cha Riadha Kenya kimeteaua wanariadha 35 watakaoshiriki makala ya 31, ya michezo ya Olimpiki jijini Paris Ufaransa baina ya Julai 26 na Agosti 11 mwaka huu.

Timu hiyo inawajmuisha wanariadha chipukizi na wale waliobibea imechaguliwa Jumamosi, kufuatia kukamilika kwa majaribio ya kitaifa ya siku mbili.

Mshikili wa rekodi ya dunia ya mita 10,000 Beatrice Chebet na bingwa mara mbili wa Olimpiki Faith Kipyegon, watashiriki mashindano mawili kila mmoja.

Susan Ejore na Nelly Chepchirchir wataungana na Faith Kipyegon katika mita 1,500, huku timu ya wanaume ikimshirikisha bingwa wa zamani wa duna kwa chipukizi Raynold Kipkorir na bingwa wa dunia mwaka 2019 Timothy Cheruiyot.

Bingwa wa dunia Mary Moraa atashiriki mita 400 pamoja na kujiunga na Lillian Odira kwenye mita 800.

Kikosi kilichotajwa ni kama kifuatavyo:

100m men
Ferdinand Omanyala

400m Women
Mary Moraa

400mH
Wiseman Were

800m women
Lillian Odira
Mary Moraa

800m Men
Emmanuel Wanyonyi
Wycliff Kinyamal
Koitatoi Kidali

1500m men
Raynold Kipkorir
Timothy Cheruiyot

1500 women
Faith Kipyegon
Nelly Chepchirchir
Susan Ejore

3000msc Women
Faith Cherotich
Jackline Chepkoech
Beatrice Chepkoech

3000msc men
Amos Serem
Simon Koech
Abraham Kibiwott

5000m women
Faith Kipyegon
Beatrice Chebet

5000m men
Ronald Kwemoi
Jacob Krop
Edwin Kurgat

10,000m women
Beatrice Chebet
Lillian Kasait
Margaret Chelimo

10,000m men
Daniel Mateiko
Nicholas Kipkorir
Bernard Kibet

Marathon Women
Peres Jepchirchir
Hellen Obiri
Brigid Kosgei
Sharon Lokedi-Reserve

Marathon men
Eilud Kipchoge
Alexander Mutiso
Benson Kipruto
Timothy Kiplangat-Reserve

Kikosi hicho kimeagizwa kuripoti kambini Jumanne ijayo kuanza mazoezi ya Olimpiki.

Website |  + posts
Share This Article