Rais William Ruto ametangaza nyongeza ya mshahara wa wafanyakazi kwa asilimia 12, katika sherehe za 61, za siku kuu ya Leba Dei.
Sherehe hizo sherehe zimeandaliwa Ijumaa katika shule ya Chavakali Boys, kaunti ya Vihiga.
Pia Rais, ametangaza nyongeza ya silimia 15, kwa mshahara wa wafanyakazi wa sekta ya kilimo.
Aidha,Ruto ametoa hakikisho la kuboresha maslahi ya wafanyakazi .
Sherehe za Leba Dei, zimeandaliwa leo kwa mara ya kwanza nje ya kaunti ya Nairobi, na zilihudhuriwa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi nchini pamoja na viongozi wakuu serikalini.