Shirikisho la soka nchini Senegal limetangaza kumtimua kocha mkuu wa Teranga Lions Pape Thiaw, na wasaidizi wake wote, kufuatia matokaeo mabovu ambapo timu hiyo ilibanduliwa katika hatua ya 32, ya Kombe la Dunia na Ubelgiji.
Aidha, Senegal ilishinda mechi moja pekee ya kundi lao mabao 5-0 dhidi ya Iraq, ndiposa ikafuzu kwa hatua ya 32 bora.
Kocha huyo anatimuliwa baada ya kuongeza mkataba wa kuifunza Teranga Lions, kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia mwaka huu.
Thiaw aliye na umri wa miaka 45, anakumbukwa sana kwa kuwaongoza wachezaji kuondoka uwanjani katika fainali ya kombe la AFCON,Januari mwaka huu kupinga penati iliyopewa wenyeji Morocco.