Pipeline kuvaana na APR fainali ya Zone 5

Dismas Otuke
1 Min Read

Mabingwa watetezi Kenya Pipeline watazundua uhasama na APR kutoka Rwanda kwenye fainali ya taji ya Africa Zone V mjini Kampala Uganda.

Vidosho wa Pipeline walifuzu kwa fainali baada ya kuwazaba wenyeji Sports-S seti tatu kwa bila katika nusu fainali jana.

KPC walisajili ushindi wa 25-19, 25-22, na 25-15 wakijivunia kutoshindwa mechi hata moja tangu kuanza kwa mashindano hayo.

APR nao walitinga fainali kufuatia ushindi wa seti zizo hizo 3-0 dhidi ya Uganda alama 25-16, 25-11, na 25-10.

Share This Article
Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *