Kasisi mkuu wa kanisa la kianglikana, Jackson Ole Sapit, amepiga marufuku wanasiasa kuongea katika makanisa ya ACK kote nchini.
Ole Sapit amesema wanasiasa watauruhusiwa kuzungumza na waumini nje ya kanisa baada ya ibada.
Aidha, kasisi huyo amesema kanisa lake kamwe halitatangaza sadaka inayotolewa kanisani na waumini au washirika.
Ole Sapit ametangaza haya Jumapili katika kanisa lake wakati wa ibada iliyohudhuriwa na aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, Kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka, Kiongozi wa chama cha DAP-K Eugene Wamalwa na Gavana wa Nairobi Johnson Sakaja miongoni mwa wanasiasa wengine.
.