Ni kufa kupona vipusa wa Kenya wakimenyana na Gambia kufuzu WAFCON

Mchuano huo utachezewa nchini Senegal ambapo Kenya wanalenga kufuzu kwa  kipute hicho kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2016.

Dismas Otuke
1 Min Read

Timu ya taifaya Kenya ya soka ya wanawake Harambee Starlest imeratibiwa kuchuana Gambia, katika marudio ya raundi ya pili kufuzu kwa fainali za Kombe la mataifa ya Afrika (WAFCON) mwaka ujao nchono Morocco.

Starlets chini ya ukufunzi wa Beldine Odemba  ilishinda mkumbo wa kwanza mabao 3-1, wiki jana na wanahitaji sare tu au hata kupoteza bao 1-0, dhidi ya wenyeji Gambia ili kufuzu kwa fainali hizo kwa mara ya pili.

Mchuano huo utachezewa nchini Senegal ambapo Kenya wanalenga kufuzu kwa  kipute hicho kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2016.

Pambano hilo litang’oa nanga saa moja usiku.

 

Website |  + posts
Share This Article