Mwanamke ajipata mashakani baada ya kumbusu msanii wa Korea Kusini

BBC
By
BBC
2 Min Read
Jin alifanya hafla ya kukumbatiana bila malipo ambapo aliwakumbatia mashabiki 1,000 mwaka jana baada ya kuachiliwa kutoka jeshi

Mwanamke Mjapani anachunguzwa na maafisa wa polisi wa Korea Kusini kwa kumbusu Jin wa BTS katika tafrija la mashabiki huko Seoul mwaka jana.

Mwanamke huyo badala ya kumkumbatia Jin kama mashabiki wengine wa BTS alimbusu msanii huyona Jin alionekana kutoridhishwa na hatua hiyo.

Tukio hilo lilisababisha hasira kwa mashabiki wengine, na mmoja wao alilalamika kwa polisi baada ya video hiyo kuenea mitandaoni.

Polisi wa Korea Kusini wamemuita mwanamke huyo, ambaye kwa sasa yuko Japan, kujitokeza kwa mahojiano kuhusu tuhuma za kumnyanyasa kijinsia Jin wakati wa tukio hilo la hadhara.

Baadaye, mwanamke huyo aliandika kwenye blogu yake na kukiri kumbusu Jin kwenye shingo yake.

BBC ilijaribu kuwasiliana na wakala wa BTS, HYBE, kwa maoni kuhusu tukio hilo.

Jin ni mshiriki wa kwanza wa BTS kutolewa kutoka huduma ya kijeshi.

Alifuatiwa na J-Hope ambaye alikamilisha huduma yake mwezi Oktoba.

Wengine wanne – V, RM, Jimin, Jungkook, na Suga – bado wanaendelea na huduma zao, na kundi linatarajiwa kuungana tena mwezi Juni 2025.

Wasanii wa K-pop wanajulikana kwa kuwa na uhusiano wa karibu na mashabiki wao kupitia njia mbalimbali za mawasiliano na matukio ya ana kwa ana.

Ni kawaida kwa wasanii kuwasiliana na mashabiki kupitia mitandao ya kijamii na matukio ya moja kwa moja ili kujenga uaminifu wa mashabiki.

Hata hivyo, mashabiki na mashirika yanaendelea kutambua baadhi ya tamaduni hatarishi za mashabiki, kama vile “sasaeng fans”, ambao mara nyingi hujishughulisha na unyanyasaji kwa wasanii wao.

TAGGED:
Share This Article
Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *