MultiChoice yaadhimisha miaka 30 katika tasnia ya filamu Kenya

Meneja Mkurugenzi wa Multichoice Kenya Nzola Miranda, alisema wamewekeza shilingi bilioni 6.5 tangu mwaka 2016 katika sekta ya filamu nchini ambazo zimewaajiri Wakenya wengi.

Dismas Otuke
1 Min Read
Kushoto hadi Kulia: Nzola Miranda, Meneja Mkurugenzi wa Managing MultiChoice Kenya; Tony Owase, Afisa Mkuu Mtendaji wa tume ya filamu nchini Kenya; na Sudi Wandabusi, mwenyekiti wa halmashauri ya tume ya filamu nchini, katika maadhimisho ya miaka 30 ya MultiChoice.

Kampuni ya Afrika Kusini ya Multichoice, iliadhimisha miaka 30 tangu kujiunga na tasnia ya runinga na filamu humu nchini .

Ili kushereherehelea miongo hiyo mitatu, Multichoice imeanzisha kampeini ya kuwatuza wateja wake ambayo itaandelea hadi Septemba 30 mwaka huu, kwa wateja wa huduma za DStv, Showmax, na GOtv.

Meneja Mkurugenzi wa Multichoice Kenya Nzola Miranda, alisema wamewekeza shilingi bilioni 6.5, tangu mwaka 2016 katika sekta ya filamu nchini ambazo zimewaajiri Wakenya wengi.

Sherehe hizo pia zilishuhudia waigizaji maarufu wa humu nchini na watayarishaji vipindi wakituzwa kwa jitihada za kuinua tasnia hiyo humu nchini.

Website |  + posts
Share This Article