Magari mawili ya kifahari yanaswa nyumbani kwa Spika wa Uganda

Haya yanajiri huku serikali ikiendesha msako mkali dhidi ya Among, kuhusiana na madaia ya ufisadi na ufujaji pesa.

Dismas Otuke
1 Min Read

Maafisa wa idara ya upelelezi jijini Kampala,Uganda, wamenasa magari mawili ya kifahari kutoka nyumbani kwa Spika wa bunge la kitaifa anayeondoka Anita Among siku ya Jumatano.

Gari la tatu lililopatikana na kubebwa kutoka eneo la Nakasero nyumbani kwa Among,lilikuwa la Mercedes-Maybach, huku la nne likiwa aina ya Lexus -UBP 704Y.

Magari hayo yanaongezea kwa yale ya Roll Ryce, na Range Rover, yaliyokamatwa na kubebwe wiki jana.

Haya yanajiri huku serikali ikiendesha msako mkali dhidi ya Among, kuhusiana na madai  ya ufisadi na ufujaji pesa.

Masaibu na shinikizo hizo zimemlazimu Among, ambaye ni mumewe Rais wa Shirikisho la kandanda nchini Uganda, Moses Magogo, kujiondoa kutetea kiti cha Spika.

Share This Article