Kenya yapangwa na Uingereza,Fiji na Afrika Kusini msururu wa Bordeaux Sevens

Dismas Otuke
1 Min Read

Timu ya Kenya ya raga kwa wachezaji saba kila upande -Shujaa,imejumuishwa kundi A, katika msururu wa tatu na wa mwisho wa Bordeaux, utakaondaliwa mwishoni mwa juma hili Juni 5 na 7, nchini Ufaransa.

Kenya itakabiliana na Fiji,Afrika Kusini na Uingereza katika kundi hilo.

Shujaa inahitaji kumaliza miongoni mwa timu nane bora katika mkondo huo, ili kufuzu kwa mashindano ya dunia msimu ujao.

Kundi B linajumuisha Uruguay,Uhispania,Marekani na Australia huku kundi la mwisho la C, likiwa na Argentina,New Zealand,Ufaransa na Ujerumani.

Shujaa ni ya nane katika msimamo wa dunia kwa pointi 14,zikiwemo 8 za msururu wa Hongkong na sita za msururu wa wikendi iliyopita huko Valladolid,Uhispania.

Share This Article