Kenya yakumbatia uwekekazaji wa Qatar katika sekta za mafuta na mbolea

Dismas Otuke
1 Min Read

Serikali ya Kenya imekubali pendekezo la serikali ya Qatar kuwekeza nchini katika miradi ya mafuta ,gesi,na mbolea huku nchi zote zikilenga kutanua mawanda ya ushirikiano  na  kuhuisha utangamano.

Haya yamefichuliwa Jumatatu na Waziri wa biashara Salim Mvurya, alipokutana na  balozi wa Kenya nchini Qatar Mohammed Mutair al Enazi afisini mwake.

Mvurya na Mutair walijadilaina kwa kina kuhusu ushirikiano wa kidiplomasia  baina ya mataifa hayo mawili  na njia za kuimarisha ushirikiano wa kibiashara.

Website |  + posts
Share This Article