Thursday, 16 Apr 2026

Welcome to the official Kenya Broadcasting Corporation (KBC) News YouTube channel.

 
Explore Now
KBC Swahili
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
    • Habari Kuu
  • Back to KBC
  • Kimataifa
  • Habari Kuu
  • Michezo
  • Burudani
  • Biashara
  • Habari
KBC SwahiliKBC Swahili
Font ResizerAa
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
  • Back to KBC
Search
  • Habari
  • Biashara
  • Burudani
  • Michezo
  • Kimataifa
    • Habari Kuu
  • Back to KBC
Have an existing account? Sign In
Follow US
© 2022 Foxiz News Network. Ruby Design Company. All Rights Reserved.
Home Blog Kanye West afuta akaunti yake ya mtandao wa X
Burudani

Kanye West afuta akaunti yake ya mtandao wa X

Aliafikia hatua hiyo baada ya kuchapisha maneno kadhaa yanayoashiria chuki dhidi ya Wayahudi na wengine.

Marion Bosire
February 10, 2025 8:40 am
By Marion Bosire
Share
2 Min Read
SHARE

Mwanamuziki Kanye West amefuta akaunti yake ya mtandao wa X baada ya kuchapisha maneno kadhaa yanayoashiria chuki dhidi ya Wayahudi.

Awali, usimamizi wa mtandao wa X ulikuwa umeweka onyo la maudhui ya kutiliwa shaka kwenye akaunti hiyo ya Kanye.

Kanye alianza kuchapisha maneno hayo ya kusikitisha Ijumaa Februari 7, 2025 ambapo aliandika maneno kama vile kukiri kuwa mwanachama wa Nazi.

Aliandika pia kwamba haamini yeyote ambaye ni Myahudi na kwamba aliandika maneno hayo akiwa hajanywa pombe hata kidogo.

West aliyebadili jina na kuwa Ye mwaka 2022, aliendelea kuchapisha taarifa zisizo nzuri hatua iliyosababisha watu kadhaa kama vile David Schwimmer kumtaka mmiliki wa X Elon Musk kumpiga Ye marufuku.

Schwimmer alisema kwamba Ye amerejelea hulka yake ya mwaka 2022 akisema kwamba hawawezi kumkomesha kusema anayoyasema lakini wanaweza kumnyima jukwaa la kutoa maoni yake.

Pallaso asema tamasha la London litafana hata bila yeye
50 Cent ashtakiwa na mpiga picha
Lupita Nyong’o ateuliwa kiongozi wa jopo la waamuzi la tamasha ya filamu ya Berlin
Mheshimiwa Mwinjuma amzuru msanii mkongwe Mzee Zorro

Alishangaa ni kwa nini Kanye West ambaye ana wafuasi milioni 32.7 kwenye mtandao wa X idadi ambayo ni mara mbili ya idadi jumla ya wayahudi anakwazwa na uwepo wao.

Schwimmer ambaye ni mwigizaji anasema matamshi ya Ye yanasababisha uhasama halisi dhidi ya wayahudi na hajui ni lipi baya zaidi kuliko lingine kati ya aliyoyachapisha Kanye.

West alianza kudhihirisha hulka ya kutopendelea wayahudi Disemba mwaka 2022 wakati alisema kwamba anampenda Hitler katika mahojiano na Alex Jones kwenye kipindi show Infowars.

Usemi wa Ye ulisababisha kampuni kadhaa zilizokuwa zikishirikiana naye kama vile Adidas, GAP na Balenciaga zikomeshe mikataba na yeye.

TAGGED:Antisemitic postsDavid SchwimmerElon MuskKanye WestX Account
Share This Article
Email Copy Link Print
Previous Article Meneja wa Jux amtakia mema kwenye ndoa
Next Article Kenya kuimarisha zaidi ushirikiano na nchi za kigeni, aahidi Rais Ruto

You May also Like

Burudani

Weasel Manizo na mkewe wapigana tena

September 24, 2025
Burudani

Tory Lanes katika hali dhabiti baada ya kuchomwa kisu gerezani

May 13, 2025
Burudani

Shiksha Arora aondoka KBC

July 20, 2024
Burudani

Ali Kiba, Juma Jux wamwomboleza Raila Odinga

October 15, 2025
Show More
  • More News:
  • Kenya
  • William Ruto
  • CAF
  • Tanzania
  • President William Ruto
  • Uganda
  • DCI
  • FKF
  • Rais William Ruto
  • Israel
  • Nigeria
  • USA
  • Raila Odinga
  • Musalia Mudavadi
  • EACC
  • FIFA
  • Rigathi Gachagua
  • DRC
  • ODM
  • IEBC
KBC Swahili

Information You Can Trust: Stay instantly connected with breaking stories and live updates. From politics and technology to entertainment and beyond, we provide real-time coverage you can rely on, making us your dependable source for 24/7 news.

Youtube Medium Rss

About Company

  • Contact Us
  • Advertise with US
  • Complaint
  • Privacy Policy
  • Cookie Policy
  • Submit a Tip

Real-time Updates on the Latest Stories!

© Kbc Swahili.  All Rights Reserved. 2025

Welcome to Foxiz
Username or Email Address
Password

Lost your password?