Idadi ya waliofariki kwenye tetemeko la ardhi nchini Japan imefika 13, huku wanajeshi na maafisa wa kushughulikia dharura wakiendelea kuwatafuta manusura kwenye vifusi vya majengo.
Huduma za treni na huduma kwenye baadhi ya viwanja vya ndege zimesitishwa, serikali ikiendelea kukadiria uharibifu uliosababishwa na tetemeko hilo la kipimo cha 7.1 kilichokumba eneo la Kumamoto, kusini mwa Japani.
Waziri Mkuu wa Japan, Sanae Takaichi, amesema watu kadhaa hawajulikani walipo na huenda wamekwama kwenye vifusi wakisubiri kuokolewa.
“Kuna watu ambao wanasubiri kuokolewa na muda unazidi kuyoyoma….tutaenda sote kuwatafuta na kuwaokoa watu wengi iwezekanavyo,” alisema Takaichi.
Takriban nyumba 36,900 hazina umeme, nyumba 9,500 zikikosa umeme, huku mitanao ya mawasiliano ikikatika katika baadh ya sehemu, hayo ni kwa mujibu wa msemaji wa serikali Minoru Kihara.