Derby ya 99 ya Mashemeji kati ya mahasimu wa jadi AFC Leopards na Gor Mahia itasakatwa Jumapili Aprili 26 katika uwanja wa kitaifa wa Nyayo.
Vinara wa Ligi Gor watalenga kutoshindwa derby ya pili msimu huu baada ya Ingwe kushinda mkondo wa kwanza goli moja kwa bila Disemba mwaka jana.
Mchuano huo utabaini uwezo wa aidha Gor au Leopards kushinda taji la ligi kuu ,Kogalo wakiwa kileleni kwa alama 58 tatu zaidi ya watani wao walio katika nafasi ya pili zikisalia mechi sita msimu ukamilike.
Katika mechi 98 za awali kila timu imeshinda mechi 34 na 29 kumalizikia sare.
Tiketi za mechi hiyo zinauzwa kwa shilingi 300,500,1,000 na 2,000.