Chuo Kikuu cha Moi kimetangaza kuwa kitawatimua Wahadhiri wakuu 75, huku kikitangaza kujaza nafasi zao na Wahathiri wasio wa kudumu.
Hatua hiyo imekilazimu chama cha Wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma nchini (UASU) kukimbia mahakamani kupinga hatua hiyo.
UASU inasema chuo hicho kinatumia hali ya uhaba wa pesa unaokikabili kuwafurusha Wahadhari wenye tajriba.
Chuo kikuu cha Moi kimeanza mchakato wa kuwatimua Wahadhari wa kudumu na wenye tajriba huku kikiwaajiri Wahadhiri wasio wa kudumu .