China imesema itapambana vilivyo na nyongeza mpya ya ushuru kutoka kwa Marekani huku mataifa hayo mawili yenye nguvu zaidi kiuchumi duniani yakiwa karibu kuingia katika vita vikali vya kibiashara.
China imeishutumu Marekani kwa manyanyaso baada ya Rais Donald Trump kusema atatangaza nyongeza nyingine ya asilimia hamsini juu kwa bidhaa kutoka China iwapo nchi hiyo haitabatilisha uamuzi wake wa kuziongezea ushuru bidhaa za Marekani.
Kwa upande wake wizara ya biashara ya Beijing imesema kuwa haitakubali kamwe ‘’kushinikizwa na Marekani’’ na kuapa itapigana hadi mwisho.
Ushuru huo mpya unaweza kuacha baadhi ya makampuni ya Marekani yanayoleta bidhaa fulani kutoka China yakikabiliwa na ushuru wa asilimia 104%.
Licha ya Vietnam kuathirika zaidi na ushuru wa Trump, Waziri Mkuu wa Vietnam Pham Minh Chinh anasema nchi hiyo itanunua bidhaa zaidi kutoka Marekani, zikiwemo bidhaa zinazotumika kwa usalama na ulinzi.
kwa uagizaji wa magari kutoka Japani na kile kinachojulikana ushuru wa asilimia 24% kwa bidhaa zingine za Japani.
Rais Trump pia amesema hana nia ya kusitisha nyongeza alizotangaza kwa karibu kila nchi duniani licha ya masoko ya hisa kuporomoka.