Iran yaonya majirani kutojiunga na vita vya kiuchumi vya Marekani

Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran Mohsen Rezaei alitoa onyo hilo katika mahojiano.

Marion Bosire
2 Min Read

Iran imetishia kuchukulia kama maadui, mataifa jirani na kulenga maslahi yao iwapo yatajiunga na kampeni ya Marekani ya kudhoofisha uchumi wake.

Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran Mohsen Rezaei alitoa onyo hilo katika mahojiano ya Jumamosi na shirika la utangazaji la serikali, IRIB.

“Tunaziambia nchi zote jirani zisiunge mkono vita vya kiuchumi vya Marekani. La sivyo, tutazichukulia kama maadui,” Rezaei aliiambia IRIB.

Kauli zake zimekuja baada ya vitisho vya kiuchumi kutoka kwa utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump kuongezeka.

Jumatano, Trump alitangaza kwamba serikali yake itafanya operesheni kali zaidi ya kiuchumi kuwahi kufanywa dhidi ya Iran, ikiwa ni sehemu ya uhasama unaoendelea kati ya nchi hizo mbili.

Marekani na Israel zimekuwa katika vita na Iran tangu Februari 28, wakati washirika hao wawili walianzisha mfululizo wa kwanza wa mashambulizi dhidi ya Tehran.

Mbali na kutishia uchumi wa Iran wiki hii, Trump aliahidi madhara makubwa ya kiuchumi kwa nchi yoyote itakayoipa Iran aina yoyote ya msaada wa kujiokoa.

Waziri wake wa fedha, Scott Bessent, alirudia vitisho hivyo siku iliyofuata.

Katika mahojiano ya Jumamosi, Rezaei alielezea mkakati wa Iran katika eneo hilo kuwa wa hatua tatu, ambao ungeanza kwa juhudi za kupunguza mvutano na nchi jirani.

“Kwanza tunafanya mazungumzo. Kisha tunajaribu kuwatenganisha na Marekani kwa kutumia lugha ya kirafiki, kwa sababu kwa kweli hatutafuti kupanua vita,” alisema.

TAGGED:
Share This Article