Omdurman ya Sudan yatwaa Ligi Kuu Rwanda

Klabu hiyo ilizuru uwanja wa Hilal, ambapo itacheza mechi kadhaa za Ligi ndogo zitakazoiwezesha kushiriki Ligi ya mabingwa msimu ujao.

Dismas Otuke
1 Min Read

Klabu ya Al Hilal Omdurman, kutoka Sudan, ndio  mabingwa wa Ligi Kuu nchini Rwanda, msimu wa mwaka 2025/2026.

Al Hilal walirejea nyumbani Khartoum, mapema wiki hii baada ya kunyakua taji ya Ligi kuu Rwanda, kuanza maandalizi kwa Ligi ya Mabingwa  Afrika,msimu ujao.

Klabu hiyo ilizuru uwanja wa Hilal, ambapo itacheza mechi kadhaa za Ligi ndogo zitakazoiwezesha kushiriki Ligi ya mabingwa msimu ujao.

Omdurman wamezoa alama 73 kutokana na mechi 31, ikisalia michuano mitatu kukamilisha msimu wa Ligi Kuu Rwanda.

Share This Article