Mahakama kuu ya Kenya imeamrisha kampuni ya serikali ya usambazaji kawi ya Ketraco, kulipia kampuni ya Ufaransa shilingi milioni 220, kutokana na mradi uliokwama wa nishati ya upepo wa Loiyangalani-Suswa.
Pia mahakama hiyo ilipuuzilia mbali ombi la kampuni hiyo ya Enterprise Generale Malta Forests, la kutaka fidia ya shilingi milioni 500, kwa kupotezewa muda baada ya kushindwa kuthithibitisha.