Mkenya Sabastian Sawe ameandikisha rekodi mpya ya Dunia katika mbio za marathon ya saa 1 dakika 59 na sekunde 35,akivunja rekodi ya marehemu Kelvin Kiptum ya saa 2 na sekunde 35, iliyoandikishwa mwaka 2023.
Sawe ameweka rekodi hiyo Jumapili alipohifadhi taji yake ya mwaka jana ya London Marathon .
Mwanariadha huyo aliye na umri wa miaka 30, ndiye mwanaume wa kwanza kukamilisha mbio za marathon chini ya saa 2.
Mwethiopia Yomif Kejelcha amemaliza wa pili kwa saa 1 dakika 59 na sekunde 41, huku Mganda Jacob Kiplimo akichukua nafasi ya tatu kwa muda wa saa 2 na sekunde 28.
Amos Kipruto alichukua nafasi ya tatu huku Mkenya mwingine Geofrey Kamworor akiambulia nafasi ya nane.