Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) limetangaza ugonjwa wa Ebola, kuwa dharura katika mataifa ya Uganda na Jamhuri ya Demokrasia ya Congo ,baada ya kuripotiwa kwa vifo 80.
WHO imesema kuwa Ebola ambao husababishwa na virusi vya Bundibugyo sio janga lakini mataifa yanayopakana na DRC yako katika hatari kubwa ya kuambukizwa .
Umoja wa mataifa umesema kando na vifo 80 vilivyothibitishwa kuna visa 246, ambayo vimeripotiwa DRC, baada ya uchunguzi wa maabara.
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo imeripoti visa vya ugonjwa wa Ebola, katika eneo la Bunia,Mkoani Ituri na kisa kingine kuripotiwa mjini Kinsasha.
Nchini Uganda kumeripotiwa vifo viwili kutokana na ugonjwa wa Ebola, kutoka kwa abiria waliokuwa wakiwasili kutoka DRC.