Wahudumu wa afya watoa ilani ya mgomo ya wiki mbili

Mgomo huo unatarajia kulemaza huduma za afya hususan katika hospitali za umma kote nchini, ambazo hutegemewa sana na kina yahe.

Dismas Otuke
1 Min Read

Wahudumu wa afya nchini  wametishia kugoma  endapo serikali  haitatimiza matakwa yao ndani ya siku 14 zijazo.

Vyama mbalimbali vinavyowakilisha wahudumu wa afya tayari vimetoa notisi za mgomo huku mgomo wa wastawishaji afya ya jamii( UHC), ukiingia mwezi wa tatu.

Baadhi ya matakwa  ya wahudumu wa afya  ni   pamoja na; uainishaji wa mishahara  na tume ya kuratibu mishahara SRC,kuajiriwa kwa kwa kandarasi za kudumu kwa wastawishaji wa afya ya jamii na kulipwa malipo yao ya kuhitimisha kandarasi kwa kipindi walichohudumu.

Mgomo huo unatarajia kulemaza huduma za afya hususan katika hospitali za umma kote nchini, ambazo hutegemewa sana na kina yahe.

Website |  + posts
Share This Article