UN yapunguza msaada wa chakula kwa Ukingo wa Magharibi na Gaza

WFP ilisema kwamba vikwazo vikubwa vya kifedha vimelazimisha kupunguzwa kwa msaada.

Marion Bosire
2 Min Read

Shirika la Mpango wa Chakula Duniani, WFP limeonya kwamba linalazimika kupunguza kwa nusu kiwango cha msaada wake katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa huko Gaza kutokana na matatizo ya ufadhili.

Shirika hilo la Umoja wa Mataifa lilisema Jumanne kwamba vikwazo vikubwa vya kifedha vimelazimisha kupunguzwa kwa msaada, kutoka kuwasaidia watu 400,000 hadi 200,000.

Mashirika ya kimataifa ya misaada kote duniani yamekuwa yakikabiliwa na uhaba wa fedha huku Marekani ikiongoza katika kupunguza kwa kiasi kikubwa msaada sawa na mataifa mengine ya Magharibi.

Kuanzia mwezi huu, msaada wa chakula unaotolewa kwa familia katika Ukingo wa Magharibi kwa njia ya fedha taslimu, vocha, chakula, mipango ya kujikimu kiuchumi na huduma za lishe zitapunguzwa, WFP ilisema katika taarifa.

Iliongeza kuwa ukosefu wa fedha pia unaathiri shughuli za WFP huko Gaza.

Shirika hilo la Umoja wa Mataifa linakadiria kuwa watu 900,000 katika Ukingo wa Magharibi hawana uhakika wa kupata chakula cha kutosha.

Mkurugenzi wa WFP nchini Palestina, Shaun Hughes, alisema WFP “inawapa kipaumbele watu walio katika mazingira hatarishi zaidi huku ikipunguza msaada kwa wengine licha ya mahitaji yaliyoenea.”

Huko Gaza, WFP inawasaidia watu milioni 1.5, “wakiwemo watu milioni moja wanaopokea msaada wa chakula kila mwezi,” shirika hilo lilisema.

Msemaji wa WFP kwa maeneo ya Palestina, Claire Nevill, aliiambia wanahabari kwamba shirika hilo limeanza kupunguza msaada wa fedha kwa takribani familia 75,000 huko Gaza.

Share This Article