Ujerumani yafuzu raundi ya 32, baada ya kuhemeshwa na tembo wa Ivory Coast

Nguvu mpya Deniz Undav aliwakomboa Ujerumani, kwa bao la dakika ya 68, kabla kuongeza la pili dakika ya 94.

Dismas Otuke
1 Min Read

Ujerumani ilikuwa timu ya tatu kujikatia tiketi kwa awamu ya 32 bora katika Kombe la Dunia,baada ya kutoka nyuma na kuilaza Ivory Coast mabao 2-1,katika mchuano wa kundi E, uliosakatwa Jumamosi usiku mjini Toronto,Canada.

Ivory almaarufu the Elephants walichukua uongozi kunako dakika ya 30 kupitia kwa mahodha Frankie Kesie huku magoli mawili ya Wajerumani yakikataliwa.

Nguvu mpya Deniz Undav aliwakomboa Ujerumani, kwa bao la dakika ya 68, kabla kuongeza la pili dakika ya 94.

Kufuatia ushindi huo Ujerumani wamejihakikishia kuongoza kundi hilo kwa pointi 6 wakifuatwa na Ivory Coast kwa pointi 3, huku Ecuador na Curacao waliotoka sare tasa mapema Jumapili wakiwa na alama moja kila moja.

Share This Article