Tanzania yaapa kufungia bidhaa na mazao ya kilimo kutoka Afrika Kusini na Malawi,kulipiza kisasi

Serikali ya Tanzania imekuwa  iking'ang'ana kuuza bidhaa zake  zikiwemo ndizi katika soko la Kusini mwa Afrika.

Dismas Otuke
1 Min Read

Serikali ya Muungano wa Jamhuri ya Tanzania, imeapa kulipiza kisasi na  kupiga marufuku bidhaa za kilimo na mazao  kutoka Afrika Kusini na Malawi, kulipiza kisasi baada ya mataifa hayo kuiwekea Tanzania vikwazo.  

Tanzania imesema itaweka vikwazo hivyo kuanzia tarehe Aprili 23.2025, kulingana na taarifa ya Waziri wa Kilimo Hussein Bashe.

Serikali ya Tanzania imekuwa  iking’ang’ana kuuza bidhaa zake  zikiwemo ndizi katika soko la Kusini mwa Afrika.

Aidha Waziri amewaarifu wakulima kusitisha kupakia bidhaa zao zinazopaniwa kuuzwa katika masoko hayo ya Kusini mwa Afrika hadi hali itakapokuwa shwari.

Website |  + posts
Share This Article