Shakib Cham, ambaye ni mfanyibiashara na mume wa Zarina Hassan amesema kwamba sasa anataka kupigana ndondi na wanamuziki wa Uganda Pallaso na Alien Skin.
Cham, mwanasoshalaiti ambaye katika siku za hivi karibuni ameingilia mashindano ya ndondi ya kibiashara yanayodhaminiwa na makampuni, amewataja Pallaso na Alien Skin kama watu anaotaka kuwaalika kwa mapambano ya ngumi katika siku za karibuni.
Mwisho wa wiki, Shakib Cham aliboresha rekodi yake ya ndondi kwa ushindi wa mwondoano dhidi ya Barista Timo katika pambano lililofanyika Kansanga.
Shakib Cham sasa anaangalia mbele na katika mahojiano, alieleza nia yake ya kupigana na watu kama Pallaso na Alien Skin, akiamini kuwa wawili hao wangekuwa wapinzani wazuri katika kuendeleza michezo wa ngumi ya makampuni nchini Uganda.
Kimataifa, Shakib angekaribisha fursa yoyote ya kupigana na watu kama Ashton Hall na Jake Paul.
“Ninawatazama wapinzani wanne. Kimataifa, watu kama Jake Paul na Ashton Hall. Nikipewa nafasi ya kuingia ulingoni na watu kama wao, nitaikubali kwa mikono miwili. Nawafuata kwenye Snapchat,” alisema Shakib akiongeza kwamba hilo lingeongeza thamani katika mchezo wa ndondi.
Kiwango cha ndani, nafasi yoyote ya kuwaalika Pallaso na Alien Skin kushiriki katika ndondi za makampuni alisema, itakuwa jambo zuri.
Shakib alifichua kwamba Alien Skin ni bondia anayependa sana ndondi, lakini anajikita zaidi kwenye muziki na kwamba akikubali pambano la makampuni, itakuwa faida kwa mchezo huu.
“Pia bado nina hamu ya marudiano na mtu pekee aliyewahi kunishinda hadi sasa. Nitakuwa tayari wakati wowote atakapokubali marudiano hayo” alimalizia Shakib.