Serikali yatangaza bei ya mbegu za mahindi

Martin Mwanje
1 Min Read
Dkt. Kipronoh Ronoh - Katibu katika Wizara ya Kilimo

Wakulima wana kila sababu ya kutabasamu baada ya serikali kutangaza bei za mbegu za mahindi kwa mwaka 2025/2026. 

Katibu katika Wizara ya Kilimo Dkt. Kipronoh Ronoh anasema serikali imetenga shilingi bilioni 2 kwa mpango wa utoaji ruzuku kwa mbegu za mahindi katika mwaka wa fedha 2025/2026.

Kwenye barua aliyomwandikia Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Kenya Seed Sammy Chepsiror, Dkt. Ronoh anasema lengo ni kuhakikisha nchi inazalisha chakula kwa wingi ili kukidhi mahitaji yake.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kilo moja ya mbegu ya mahindi sasa itauzwa kwa shilingi 250, kilo 2 kwa shilingi 500, kilo 10 kwa shilingi 2,500 na kilo 25 kwa shilingi 6,000.

Tangazo hilo linakuja wakati msimu wa upanzi umepamba moto katika maeneo mengi ya nchi kufuatia ujio wa mvua.

Share This Article