Serikali yapunguza bei ya miwa kwa shilingi 250 kwa tani

Dismas Otuke
1 Min Read

Serikali imetangaza kupunguza bei ya miwa inayowasilishwa na wakulima viwandani kwa shilingi 250 kwa kila tani moja kote nchini.

Halmashauri ya sukari nchini  ilitangaza kuwa tani moja ya miwa itakuwa ikinunuliwa kwa shilingi 5,500, kutoka bei ya awali ya shilingi 5,750 kwa tani moja.

Bei hiyo mpya iliafikiwa na kamati ya muda  ya kuweka bei  kwa kuzingatia gharama ya uzalishaji,bei ya soko katika ukanda wa Afrika Mashariki  na mapendekezo ya wadau.

Pia kupunguzwa kwa bei ya miwa kumechochewa na  kupungua kwa bei ya sukari kwa gunia la kilo 50 kutoka shilingi  7,000 hadi kati ya shilingi 6,000 na shilingi 6,100 kwa sasa.

Bei ya tani moja ya miwa nchini Tanzania  ni shilingi 4,900,ilihali nchini Uganda tani moja inanuliwa kwa shilingi 4,500 za Kenya.

 

Share This Article