Rais William Ruto ameikabidhi klabu ya Migori Youth FC, basi jipya baada ya kushinda taji ya ligi kuu daraja ya kwanza (NSL),na kupandishwa ngazi kucheza Ligi Kuu msimu ujao.
Hafla hiyo imeandaliwa siku ya Jumatatu katika Ikulu ya Nairobi, na kuhudhuriwa na maafisa klabu hiyo pamoja na viongozi wa kaunti ya Migori.
Akizungumza baada ya kukutana na wachezaji wa Migori, Rais alikariri azma ya serikali yake kuboresha miundombinu ya michezo nchini ikiwemo kaunti ya Migori ili kuchochea ukuzaji vipaji.

Aliongeza kuwa basi hilo litawawezesha wachezaji wa timu hiyo kusafiri kwa mechi za Ligi kuu na pia kusafiri kwa minaajili ya mazoezi.
Rais pia alitumia fursa hiyo kuipongeza timu ya wanawake chini ya umri wa miaka 17,kufuzu kwa Kombe la Dunia kwa mara ya pili jana.
