Rais Ruto aondoka nchini kwa ziara nchini Marekani

Dismas Otuke
2 Min Read

Rais Ruto ameondoka nchini Jumapili jioni kwa ziara rasmi ya kiserikali nchini Marekani anakotarajiwa kusaini mikataba kadhaa ya ushirikiano katika sekta mbali mbali.

Ruto ataanza ziara yake Jumatatu kwa kuzuru Atlanta, Georgia atakapotembelea makavazi na maktaba ya Kirais.

Rais pia atazuru kanisa la Ebenezer Baptist kutoa heshima kwa wapiganiaji wa haki za kibinadamu waliouawa.

Kwenye ziara yake nchini Marekani Rais Ruto pia anatarajiwa kusaini mikataba kadhaa katika  kituo cha kudhibiti maradhi yaani CDC .

Siku ya Jumanne Rais atazuru chuo cha Spelman  atakapojadili mchango mhimu wa vyuo na pia mchango wa Kenya katika maendeleo ya nguvukazi na baadaye kuzuru studio za Tyler Perry kubaini fursa za ushirkiano katika sekta ya sanaa na kutembelea pia makao makuu ya kiwanda cha Coca Cola ambapo mkataba mpya wa ushirikiano unatarajiwa kutangazwa.

Baadaye Jumanne Rais atalakiwa na Meya wa Atlanta kando na  kufungua duka la  Vivo la Kenya  linalouza nguo nchini Marekani.

Jumatano Ruto na mkewe watawasili mjini Washington D.C’s ambapo watapokea makaribisho rasmi ya kiserikali,kabla ya kuhutubia mabunge yote mawili

Alhamisi Rais Ruto atafanya kikao na mwenyeji wake Joe biden  kujadiliana kuhusu mikataba kadhaa ya ushirikiano baina ya nchini hizo mbili, kabla ya kutoa hotuba kwenye ikulu ya White House.

Siku ya Ijumaa Ruto atafanya mazungumzo na makamu Rais wa Marekani Kamala Harris, kabla ya kuzuru Pentagon ambapo atajadiliana kuhusu ushirikiano katika sekta ya ulinzi na vita dhidi ya ugaidi.

Website |  + posts
TAGGED:
Share This Article