Rais wa Kenya William Ruto amefunga safari ya kuelekea nchini Italia Jumapili adhuhuri, kwa ziara rasmi ya siku tatu.
Naibu wake Kithure Kindiki na kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa Kimani Ichung’wah, walikuwa miongoni mwa viongozi wakuu serikalini waliofika katika angatua ya JKIA kumuaga Rais.
Akiwa Italia Rais anatarajiwa kusaini makubaliano ya ushirikiano ya sekta mbalimbali kati ya Kenya na Italia.