Nyangumi wa Cape Verde wakata jasho kabla ya kutinga kwota fainali ya AFCON kwa mara ya kwanza

Dismas Otuke
1 Min Read

Cape Verde  almaarufu Blue Sharks walikuwa na kibarua cha ziada kabla, ya kuwabwaga Mauritania  bao moja bila na kufuzu kwa kwota fainali ya kombe la AFCON kwa mara ya kwanza .

Kipindi cha kwanza cha  pambano hilo lililosakatwa kiwarani Félix Houphouët-Boigny Mjini Abidjan Ivory Coast, kilimalizikia sare  tasa, huku timu zote zikiwa butu katika  mashambulizi.

Hata hivyo kipa wa Mauritania  maarufu kama Simba wa Chinqueti ,Babacar Niasse  alimwangusha mshambulizi wa Cape Verde  Mohammed Adel na kuwazawidi penati zikisalia dakika 2 mechi ikamilike.

Penati hiyo iliunganishwa na nahodha wa Cape Verde Ryan Mendez katika dakika ya 88.

Nyangumi wa Cape Verde watakabaliana na mshindi kati ya Afrika Kusini na Morocco  katika hatua ya nane bora.

 

Website |  + posts
Share This Article