Melania Trump awa mke wa rais wa hivi karibuni zaidi kutoka Republican kuunga mkono utoaji mimba

BBC
By
BBC
1 Min Read
Reuters

Melania Trump anaonekana kuungana na msururu mrefu wa wake wa rais wa zamani wa chama cha Republican ambao wamejitokeza kuunga mkono haki za utoaji mimba, na hivyo kwenda kinyume na maoni ya umma ya waume zao.

Katika klipu fupi ya video inayotangaza kitabu chake kijacho, Bi Melania Trump alionyesha kuunga mkono “uhuru wa kibinafsi” wa wanawake, akielezea kama “haki muhimu ambayo wanawake wote wanayo tangu kuzaliwa”.

Hii inakuja siku moja baada ya sehemu ya kumbukumbu yake ambayo itatolewa hivi karibuni, ambapo inasemekana ana msimamo wa kuunga mkono uchaguzi ulio wazi zaidi, kuchapishwa katika ripoti ya gazeti.

Msimamo dhahiri wa Bi Trump kuhusu suala hilo unaonekana kutofautiana na msimamo wa mumewe, ambaye amejipongeza kwa kusaidia kupindua uamuzi wa kesi ya Roe v Wade, na kupinga haki ya kikatiba ya kutoa mimba.

Lakini msimamo huu wa Melania inafuatia utamaduni wa Wamarekani wa miongo kadhaa ya wake wa marais kutoka chama cha Republican ambao tangu kuamriwa kwa kesi ya Roe v Wade kwa mara ya kwanza mwaka wa 1973 ambao wamesema utoaji mimba kisheria unapaswa kulindwa.

BBC
+ posts
Share This Article