McCarthy ataja kikosi cha wachezaji 23 kwa mechi za kufuzu kombe la Dunia

Kenya ni ya nne katika kundi F kwa  pointi 6 ,pointi 9 nyuma ya viongozi Ivory Coast.

Dismas Otuke
1 Min Read

Kocha wa timu ya taifa ya Kenya,Harambee Stars  Benni McCarthy, ametaja kikosi cha wanandinga 23 kwa mechi mbili za kufuzu kwa Kombe la Dunia mwezi ujao.

Kikosi cah McCarthy kinawajumuisha wachezaji 13, walioshiriki fainali za kombe la CHAN mwaka huu.

Mshambulizi chipukizi Job Ochieng  anayepiga soka ya kulipwa katika klabu ya Real Sociadad B nchini Uhispania,  ameitwa kikosini kwa mwara ya kwanza.

Harembee  Stars itawaalika Gambia tarehe 5 mwezi ujao katika uwanja wa Kasarani katika mchuano wa kundi F, kufuzu kwa Kombe la Dunia mwaka ujao kabla ya kupimana nguvu na Ushelisheli tarehe 9 katika uo huo wa Kasarani.

Kenya ni ya nne katika kundi F kwa  pointi 6 ,pointi 9 nyuma ya viongozi Ivory Coast.

Website |  + posts
Share This Article