Mataifa 13 yafuzu kwa makala ya 23 ya kipute cha Kombe la Dunia mwaka ujao

Jumla ya mataifa 48 yatashiriki fainali za Kombe la Dunia za mwaka ujao kwa mara ya kwanza, ikiwa ongezeko kutoka idadi ya timu 32.

Dismas Otuke
1 Min Read

Mataifa 13 yamefuzu kwa makala ya 23 ya kipute cha Kombe la Dunia mwaka ujao katika mataifa ya Mexico,Marekani na Canada.

Timu zilizofuzu ni pamoja na sita ya bara Asia: Australia, Iran, Japan, Jordan, Korea Kusini, na Uzbekistan; matatu ya eneo la CONCACAF wakiwa wenyeji watatu: Canada, Mexico, na Marekani; matatu ya eneo la CONMEBOL: Argentina, Brazil, Ecuador, na New Zealand kutoka eneo la Oceania.

Jumla ya mataifa 48 yatashiriki fainali za Kombe la Dunia za mwaka ujao kwa mara ya kwanza, ikiwa ongezeko kutoka idadi ya timu 32.

Website |  + posts
Share This Article