Marekani kuwaachisha kazi wafanyakazi wa serikali

Tom Mathinji and BBC
1 Min Read

Ikulu ya Marekani inasema itaanza kuwaachisha kazi wafanyikazi wengi wa serikali ndani ya siku mbili, huku wabunge wakilaumiwa kwa kusitisha shughuli za serikali kwa mara ya kwanza katika karibu miaka saba.

Shughuli za serikali zilianza kutatizika siku ya Jumatano baada ya Republican na Democrats bungeni kushindwa kukubaliana juu ya mpango mpya wa matumizi kabla ya tarehe ya mwisho ya usiku wa manane.

Kuna dalili ndogo kwamba pande zote mbili ziko tayari kuafikiana, na kura ya kumaliza kulemaa kwa shughuli hizo ilishindikana saa chache baada ya kuanza.

Tangu wakati huo, bunge la Seneti limeahirisha vikao vyake, na hivyo kuzua hofu kwamba hatua hiyo inaweza kuendelea na kutishia mamia ya maelfu ya kazi na vile vile hatari ya kugharimu uchumi wa Marekani kwa kupotea kwa mabilioni.

Website |  + posts
Share This Article