Kongamano la Ugatuzi 2025 kuandaliwa Homa Bay

Martin Mwanje
1 Min Read
Gavana wa Homa Bay Gladys Wanga akiwa Seneta mteule Catherine Mumma
Kongamano la Ugatuzi la mwaka 2025 litaandaliwa katika kaunti ya Homa Bay kati ya Agosti 12-15, 2025. 
Hii imetangazwa leo Jumanne baada ya kukamilika kwa mkutano wa kamati inayoratibu kongamano hilo mwaka huu.
Mkutano huo ulihudhuriwa na Magavana Gladys Wanga wa Homa Bay na Mutahi Kahiga wa Nyeri miongoni mwa viongozi wengine.
Kongamano la Ugatuzi hutumiwa kupigia msasa hatua iliyopigwa katika utekelezaji wa ugatuzi tangu kuasisiwa kwake.
Mawaziri, Magavana, Maseneta, wabunge na wataalam katika nyanja mbalimbali ni miongoni mwa viongozi ambao kwa kawaida uhudhuria kongamano hilo.
Share This Article
Leave a Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *